Jeudi 28 mars 2024

Archives

Mapigano makali yazuka Mogadishu

05/05/2013 Commentaires fermés sur Mapigano makali yazuka Mogadishu

Kwa mujibu wa duru za kuaminika, serekali ya mpito ya Somalia inabaini kua wapiganaji 6 wa kundi la Al-Shabaab waliuawa hapo alhamisi disemba 8 huko Karan na Huriwa kaskazini mwa mji wa Mogadishu katika mapigano kati ya wapiganaji hao na askari wa serekali ya mpito wanaoungwa mkono na vikosi vya Umoja wa Afrika.

<doc2285|left>Mmoja kati ya wasemaji wa kundi hilo anakiri kua kuliuawa askari 9 wa serekali na wengine 4 kutoka vikosi vya Umoja wa Afrika katika mapigano hayo. Yote hayo yalianza nyakati za alfajiri bada ya askari wa serekali kushambuliwa na wapiganaji hao wa Al Shabaab. Ilibidi vikosi vya Umoja wa Afrika vilivyotumwa nchini humo kurejesha amani vitumie vifaru na zana nzito.

Wachunguzi wa mambo wanabaini kua pengine wapiganaji wa Al-Shabaab wana nia ya kurejea kwenye ngome zao za zamani mjini Mogadishu. Hayo ni baada ya Al-Shabaab kuchukuwa uamzi wa kuondoka Mogadishu hapo mwezi ogasti na serikali kutangaza kuwa inaudhibiti mji huo.

Na hapo ijuma tano wapiganaji wa Al-Shabaab walishambulia kambi ya kijeshi inayosimamiwa na vikosi vya Umoja wa Afrika katika mji wa Wadajir kusini mwa Mogadishu.

Umoja wa Afrika una vikosi takriban 9,000 mjini Mogadishu vilivyotumwa nchini humo kurejesha amani na hasa kuunga mkono serikali ya mpito. Kenya pia imetuma askari wake kusini mwa Somalia tangu mwezi Octoba, kufuatia hujuma za wapiganaji wa Al Shabaab na utekaji nyara kwenye mpaka baina nchi hizo mbili. Bunge la Kenya liliisha kubali jeshi la Kenya lijiunge na vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Somalia.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

La fin du Phénix ?

Les dés sont jetés, les carottes sont cuites : le ministre de l’Intérieur a validé les conclusions issues du congrès extraordinaire tenu à Ngozi le 10 mars par des dissidents d’Agathon Rwasa. « Nous prenons acte du rapport et des décisions prises (…)

Online Users

Total 3 845 users online