Jeudi 25 avril 2024

Archives

Mauaji ya Gatumba yalaniwa na Jumuia ya kimataifa, vyama vya siasa na mashirika ya kiraia

21/09/2011 Commentaires fermés sur Mauaji ya Gatumba yalaniwa na Jumuia ya kimataifa, vyama vya siasa na mashirika ya kiraia

Bada ya watu zaidi ya 39 kuuwawa na wengine zaidi ya 10 kujeruhiwa huko Gatumba (maghariba mwa mji wa Bujumbura) hapo ijumapili usiku katika shambulio dhidi ya kilabu lililoendeshwa na watu wenye kuvalia sare za kijeshi na za polisi na kubebelea silaha, Jumuia ya kimataifa, vyama vya siasa na mashirika ya kiraia yanazidi kulani mauaji hayo na yanaomba vyombo vya vianzishe uchunguzi ili waliohusika katika kitendo hicho waadhibiwe.

Serekali ya Burundi ilitoleya wito vyombo vya sheria ikivitaka kutoa mwanga kuhusu mauaji hayo katika muda usiozidi mwezi moja ili waliohusika katika kitendo hicho waadhibiwe na ’’ikiwa vitashindwa kutaitishwa vyombo vya sheria vya kimataifa’’, alisema hayo Rais wa Jamhuri, Pierre Nkurubnziza ambae amejielekeza huko New York kushiriki kikao kikuu cha Umoja wa Mataifa.

Kwa jumla vyama vya siasa nchini Burundi vinalani vikali mauaji hayo bila kusahau mashirika ya kiraia ambayo yanaomba walioendesha mauaji hayo ya kikatili waadhibiwa vikali. Mashirika hayo yanaomba pia kufanyike uchunguzi ili kutolewe mwanga kuhusu maiti zinazozidi kuokotwa hapa na pale.
Mashirika hayo ya kiraia ikiwa ni pomoja na APRODH, Ligue Iteka, OAG, FORSC na mengineyo yanahakikisha kua watu zaidi ya 100 waliuwawa tangu mwezi mei mwaka huu katika operesheni za kuwasaka wafuasi wa Agathon Rwasa kinara wa chama cha waasi cha zamani cha FNL. Wakati huu aliingia mafichoni bada ya madai ya uizi wa kura katika chaguzi za hapo mwaka jana zilizopelekea chama cha CNDD FDD kubuka ushindi.

Upande wa Jumuia ya kimataifa, Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon analani vikali mauaji hayo ya Gatumba. Anasema wakati Burundi ikiwa mbioni katika harakati za kuboresha amani bada ya miaka zaidi ya 10 ikiwa katika lindi la machafuko, shambulio hilo halieleweki. Umoja wa Mataifa unaomba waliohusika katika vitendo hivyo waadhibiwe kwa mujibu wa sheria huku ukitolea wito pande zote ukizitaka kutoendelea kuzozana.

« Serekali ya Umarekani inalani na inasikitishwa na mauaji hayo dhidi ya mgahawa huko Gatumba ambayo yanaonekana kua yalikusudiwa », inasema taarifa kutoka kwenye ubalozi wa Umarekani jijini Bujumbura. Serekali ya Umarekani inayiomba serekali ya Burundi ifanye kila iliwezalo ili waliotenda unyama huo wafikishwe mbele ya mahakama. Serekali ya Umarekani inaziomba pande zote kukomesha mauaji na kudumisha maridhiano.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ubelgiji, Steven Vanackere analani vikali mauaji hayo yaliyofanyika huko Gatumba katika mgahawa. Anasema kutiwa hofu na hali ya kuzuka tena machafuko nchini Burundi. « Kamwe vurugu si suluhisho kwa matatizo nchini Burundi », anazidi kusema Waziri huyo wa mambo ya kigeni wa Ubelgiji huku akiomba makundi ya wapiganaji kutia silaha chini. Waziri Vanackere anakiri kua mazungomzo ya kisiasa, maafikiano na kuliendeleza taifa bila ubaguzi kwa manufaa ya kila raia na chini ya uheshimishaji wa taasisi zilizoteuliwa na misingi ya kidemokrasi, ndio njia pekee ya kuyatanzua matatizo yanayoikabili Burundi.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

Une responsabilité de trop

« Les décisions prises par la CVR ne sont pas susceptibles de recours juridictionnels. » C’est la disposition de l’article 11 du projet de loi portant réorganisation et fonctionnement de la Commission Vérité et Réconciliation analysée par l’Assemblée nationale et le Sénat (…)

Online Users

Total 5 129 users online