Jeudi 25 avril 2024

Archives

Gatumba: Shirika la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari, RSF linaunga mkono vyombo vya habari

23/09/2011 Commentaires fermés sur Gatumba: Shirika la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari, RSF linaunga mkono vyombo vya habari

Shirika la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari, ”Reporters without Borders” linaomba Serekali ya Burundi ifutilie mbali hatua ya kuvikataza vyombo vya habari kutangaza habari kuhusu mauaji ya Gatumba kwa muda wa mwezi mzima.

Katika risala ambayo shirika hilo limemtumia Rais wa Jamhuri Pierre Nkurunziza na waziri wa habari Bii Concilie Nibigira, linabaini kua linasikitishwa na hatua hio ya kupiga marfuku katika kipindi cha mwezi mzima matangazo ya moja kwa moja au vipindi vya kisiasa kuhusu uchunguzi unaofanyika juu ya mauaji yaliyotekea hapo ijuma pili nyakati za saa mbii za usiku huko Gatumba.

Shirika hilo la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari, ”Reporters without Borders” linawaomba viongozi wa Serekali ya Burundi wafutilie mbali hatua hio ya kuwakataza wanahabari ”kuchapisha, kutowa maelezo au udadisi kuhusu uchunguzi unaofanyika juu ya mauaji ya kikatili ya Gatumba”. Shirika hilo linasema uamzi huo wa serekali ya Burundi ni ”hatua kali kupitiliza”. Linabaini kua linaunga mkono hatua iliyochukuliwa na muungano wa maredio wa kutowa habari kuhusu swala tete la usalama unaozidi kuyumbishwa nchini Burundi.

Shirika hilo la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari, ”Reporters without Borders”, linakiri kua mauaji ya kinyama yaliyoendeshwa huko Gatumba ni ya kutisha na yanaweza kuleta mvutano walakin ifahamike kua harakati za kuboresha amani haziwezi kamwe kwenda sambamba na ukiukwaji wa uhuru wa vyombo vya habari, linasema Shirika hilo. Badala ya hayo, kuna umuhimu kuhimizwe mazungumzo kati ya pande zote na raia wahakikishiwe haki yao ya kupata habari kuhusu yanayojiri nchini, linazidi kusema Shirika hilo la kimataifa la kutetea haki za wandishi wa habari ”Reporters without Borders”.

A nos chers lecteurs

Nous sommes heureux que vous soyez si nombreux à nous suivre sur le web. Nous avons fait le choix de mettre en accès gratuit une grande partie de nos contenus, mais une information rigoureuse, vérifiée et de qualité n'est pas gratuite. Nous avons besoin de votre soutien pour continuer à vous proposer un journalisme ouvert, pluraliste et indépendant.

Chaque contribution, grande ou petite, permet de nous assurer notre avenir à long terme.

Soutenez Iwacu à partir de seulement 1 euro ou 1 dollar, cela ne prend qu'une minute. Vous pouvez aussi devenir membre du Club des amis d'Iwacu, ce qui vous ouvre un accès illimité à toutes nos archives ainsi qu'à notre magazine dès sa parution au Burundi.

Editorial de la semaine

Une responsabilité de trop

« Les décisions prises par la CVR ne sont pas susceptibles de recours juridictionnels. » C’est la disposition de l’article 11 du projet de loi portant réorganisation et fonctionnement de la Commission Vérité et Réconciliation analysée par l’Assemblée nationale et le Sénat (…)

Online Users

Total 5 736 users online